Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh.Said Mtanda.Amewahamasisha wananchi wote wa mkoa wa mwanza kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Mpiga kura ambalo litatumika katika Uchaguzi wa Serikali za mitaa hivi karibuni
Amesikika hii leo Julai 05.2024 kupitia Kipindi cha Mchakamchaka Kinachoruka Jembe fm Radio Amesisitiza wananwachi wote kujitokeza kwa wingi na pia kujiandikisha ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za mitaa mwezi wa Kumi na moja (Novemba) 2024
Aidha Ameongezea kusema kuwa kuanzia Traehe 21 hadi 27 mwezi wa Nane kutakua na zoezi kubwa la wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu kwa ajili ya Uchaguzi mkuu utakao fanyika Hapo mwakani
Zaidi karibu kumsikiliza kupitia hii link hapa chini
Na Maria Makanza
