Katika kuhakikisha halmashauri inapanga na kutekeleza miradi
ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma
kwa wananchi wataalam wa manispaa ya Ilemela wametakiwa kuongeza jitihada
katika ukusanyaji wa mapato na kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ili
kufikia malengo yaliyo kusudiwa.
Rai hiyo imetolewa na Mstahiki meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe. Sarah Ng'hwani
mapema tarehe 29 Januari 2026 wakati wa mkutano wa baraza la madiwani
likijadili utekelezaji wa robo ya pili kipindi cha Oktoba - Desemba 2025/2026.
Huku akizitaka tasisi zinazosimamia viwanja vya mpira wa
miguu ndani ya jiji la mwanza vianze kukarabatiwa mapema ili kutoa nafasi kwa
timu zitakazo kuja katika mashindano ya Afcon 2027 kwa kuvitumia kama sehemu ya
mazoezi ili vitoe fursa kwa wafanya biashara wakubwa na wadogo ndani ya jiji la
mwanza Zaidi karibu kusikiliza hapa
chini