Wakati Rwanda ilipokuwa na Maonesho ya Kimataifa ya Mashariki mwa Mediterania ya Utalii na Usafiri (EMITT) jijini Istanbul mapema mwaka huu, nchi hiyo imekuwa ikilenga jambo mahsusi: kupata kufikia sehemu ya watalii milioni 300 ambao hupitia mashariki mwa Mediterania kila mwaka.
"Eneo la Mashariki mwa Mediterania, likichukuliwa kama sehemu moja ya kitalii, ni moja ya eneo kubwa duniani," Charles Kayonga, balozi wa Rwanda nchini Uturuki, ameiambia TRT Afrika. "Linapokea watalii milioni 300 kila mwaka kati ya milioni 900 kote ulimwenguni. Kwa Rwanda, ambayo inajiweka katika nafasi ya kuwa kitovu cha utalii, soko hili ni muhimu kimkakati."
Ndoto hiyo iko katika nguzo tatu: wanyamapori na bayoanuai, kutokana na sokwe wa milimani katika Mbuga ya Taifa; sekta ya mikutano na makongamano inayokuwa kwa kasi, na sifa ya kuwa nchi salama zaidi kwa wageni barani Afrika.
Kayonga anaeleza Rwanda kuwa "na uwezo mkubwa kitalii", akizungumzia kuhusu uwekezaji wa serikali katika sekta ya hoteli na miundombinu ya maeneo ya mikutano kwa kile anachokiita utamaduni wa kutoa huduma unaoimarika.
Yote haya hayawezi kufanya kazi bila muunganiko wa safari za ndege na miundombinu, na ndipo ambapo umuhimu wa Uturuki unahitajika kama moja ya nchi washirika wa muda mrefu
Shirika la Ndege la Turkish Airlines lina safari kadhaa kila wiki kutoka Kigali, kuisogeza Rwanda hadi Istanbul na kuiunganisha na bara Ulaya, Asia na kote Mediterania.Kwa wafanyabiashara, wajumbe wa mikutano na watalii wanaotaka kujiburudisha, ugumu wa kuelekea katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki isiyo na bahari umeondoka.Safari hizo za ndege zimejumuishwa katika mpango wa makubaliano karibu 30 Rais wa Uturuki Recep Tayyip ErdoÄŸan na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame wamekuwa wakishirikiana kupitia mikutano mbalimbali na kutembeleana na miaka kadhaa.
Kayonga anasema ni kutokana na umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya viongozi hao.
"Hatuwezi kuwa na uhusiano wa karibu zaidi ila kuwa na uongozi thabiti," anasema. "Rais Kagame na Rais ErdoÄŸan wameimarisha uhusiano wao."
Uhusiano huu umefanya kuwepo kwa mifumo ya makubaliano, ushirikiano wa kibiashara na kuimarisha uhusiano wa watu wa mataifa hayo mawili.
Kayonga ambaye mwenyewe amesafiri katika maeneo mengi nchini Uturuki. "Naipenda hii nchi sana. Ni nzuri na ina historia thabiti. Unasafiri sehemu unakutana na vito vya kihistoria na ushahidi wa utamaduni halisi," anasema.
Kwa Rwanda, uhakika wa mkakati huu uko wazi. Taifa dogo, barani Afrika ambalo halina bahari lenye ndoto kubwa linahitaji washirika ambao wanawaunganisha, kuleta uwekezaji na umuhimu wa kidiplomasia.
Uturuki, ambayo kitovu chake ni Istanbul, ujuzi wake katika ujenzi na sera yake ya faida kwa wote katika kuongeza ushawishi wake barani Afrika, ina sifa zote za mshirika mzuri. Iwapo kama watalii milioni 300 wataanza safari zao za kwenda kuona sokwe ni suala la kuangazia.kati ya serikali hizo mbili, huku ushirikiano katika utalii ukiwa muhimu zaidi.
