Maandamano Kenya dhidi ya utekaji nyara

 

Polisi katika mji mkuu wa Kenya Nairobi wamerusha mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakiandamana siku ya Jumatatu kupinga kile wanachosema kuwa ni wimbi la utekaji nyara usioelezeka wa wakosoaji wa serikali.

"Kumekuwepo na matukio kumi na tatu (13) zaidi ya utekaji nyara au kupotea kwa watu katika kipindi cha miezi mitatu na kufanya jumla ya kesi 82 kuanzia Juni 2024," Tume ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu ya Kenya imesema katika taarifa.

Kesi saba za utekaji nyara za hivi karibuni ziripotiwa katika mwezi wa Disemba 2024 ambapo sita kati yao wakiwa bado hawajulikani walipo, hivyo kufikisha idadi ya watu 29 ambao hawajapatikana tangu Juni 2024.

Mashirika ya usalama nchini Kenya yamelaumiwa. Hata hivyo, huduma ya taifa ya polisi na kitengo cha makosa ya jinai zimekana tuhuma hiyo.

Mamlaka za Kenya zimesema kuwa serikali haikubaliani na wala haishiriki katika mauaji ya kiholela au utekaji nyara.

Baadhi ya makundi ya vijana waliandamana katikati mwa jiji la Nairobi huku wengine wakipanga kukaa na kuimba kauli mbiu dhidi ya serikali, huku baadhi wakiwa na mabango ya kukashifu kuzuiliwa kuandamana kinyume cha sheria.

Msemaji wa Polisi wa Taifa hakujibu mara moja ombi la kutoa maoni yake juu ya maandamano ya Jumatatu.

Matukio hayo ya utekaji nyara yalifuatia maandamano ya kuipinga serikali yaliyoanza Juni mwaka huu.

Hapo awali yalilenga kubatilisha mapendekezo ya nyongeza ya ushuru, maandamano hayo hatimaye yalibadilika na kuwa vuguvugu lililokumba migawanyiko ya kitamaduni ya Kenya, na kuwa tishio kubwa kwa serikali ya Rais aliye madarakani William Ruto.

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post