TATIZO LA UMEME MDOGO LAPATA UTATUZI KWA WAKAZI WA BUSWELU MWANZA.ENG MATHAYO

Wakazi wa Mtaa wa busenga kata ya Buswelu wilaya ya Ilemela,Wanakwenda kuondokana na tatizo la uhaba wa Umeme wakutosha katika Mtaa wao wenye zaidi ya Kaya 1800 na Wananchi wapatao zaidi ya 3000.Eneo lao limekua na changamoto ya muda mrefu la kua na Umeme mdogo jambo ambalo linawafanya washindwe kupiga hatua ya kimaendeleo kutokana na changamoto hiyo


Kwa Upande wake Meneja  TANESCO Mkoa wa Mwanza Eng. Godlove Mathayo amesema eneo la busenga ambalo lilikuwa na changamoto ya ukosefu wa umeme kwa muda mrefu Sasa limepata ufumbuzi kwa sababu bajeti imetoka na jambo hilo litatekelezwa hivi karibuni.

Ameyasema hayo mapema hii Leo huku akisema kuwa bajeti iliyotolewa ni sh milioni 40 ambayo itatosha kurekebisha matengenezo yote.


Aidha amewashukuru wananchi wote kwa kujitoa na kuwa wavumilivu kwa kipindi chote Cha changamoto hiyo ya umeme,na ndani ya mwezi Novemba mwaka huu kazi itakua imekwisha


Kwa Upande wake Diwani wa kata ya buswelu Sarah Paul Ng'wani  amemshukukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samia Suluh Hassan kwa kutenga fedha hizo ambazo ni sh milioni 40  kwa ajili ya matengenezo na kuwaona wakazi ya busenga kata ya Buswelu na kuwafikia kwa ajili ya kuwatatulia tatizo hilo lililodumu kwa muda mrefu.


Aidha amemshukuru meneja wa TANESCO  kwa kufikia na kuwatatulia changamoto hiyo ya ukosefu wa umeme iliyowasumbua kwa muda mrefu.

Pia amewaomba wananchi wote kutunza miundombinu ya umeme na kuilinda na pia kuwa waangalifu Ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Mwenyekiti wa mtaa wa Busenga aliyemaliza muda wake,Shokha Mhango amewashukuru TANESCO kwa kujitoa na kuwafikia Ili kuwatatulia changamoto ya ukosefu wa umeme ambayo imewasumbua kwa muda mrefu.


Ameyasema hayo na kuwaasa wananchi wote kufanya kazi kwa bidii kwani walikuwa hawafanyi kazi kwa sababu ya ukosefu wa umeme.

Aidha amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samia Suluh Hassan kwa kuwakumbuka na kusikia maombi Yao.


Sambamba na hayo wananchi wameiomba serikali kuwasaidia kuwafungia umeme katika shule ya msingi Busenga kwani itasaidia watoto kujifunza zaidi kwa vitendo.

Wameahidi kuitunza miundombinu Ili iweze kudumu kwa muda mrefu kwa ajili ya matumizi Yao ya kujipatia kipato.
















NA MARIA MAKANZA
Post a Comment (0)
Previous Post Next Post