Somalia na Kenya zakubaliana kuhusu kikosi kipya cha AU

 

Kenya na Somalia zimekubaliana kuhusu umuhimu wa kuundwa kwa kikosi kipya cha usalama nchini Somalia chini ya Umoja wa Afrika, yaani 'AU Led Mission in Somalia', AUSSOM.

Hii ni kulingana na taarifa ya pamoja iliyotolewa na nchi hizo mbilii baada ya Rais wa Somalia Sheikh Mohamud kukutana na Rais wa Kenya Willim Ruto nchini Kenya.

"Wakuu wa nchi walikaribisha kuanzishwa kwa ujumbe mpya wa Umoja wa Afrika wa kusaidia na kuleta utulivu nchini Somalia, AUSSOM ambao utaendeleza mafanikio ya mtangulizi wake Ujumbe wa Mpito wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (ATMIS)," taarifa hiyo ya pamoja ilisema.

"Viongozi walikubaliana kuwe na kipindi cha mpito cha majukumu ya usalama kutoka ATMIS hadi AUSSOM ambayo imepangwa kuaza januari 1, 2025," taarifa iliongezea.

Agosti 2024, Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, liliidhinisha pendekezo la kuunda Ujumbe wa Kusaidia na Kuleta Utulivu wa AU nchini Somalia (AUSSOM).

Itachukua nafasi ya Kikosi cha AU cha Mpito nchini Somalia (ATMIS), ambayo ilichukua nafasi ya ujumbe wa kwanza wa nchi hiyo (AMISOM) mnamo Aprili 2022.

Baraza la Amani na Usalama la Afrika lilisema uamuzi huo ulifuatia

mashauriano kwa ya kina na ATMIS, serikali ya Somalia, Umoja wa Mataifa na washirika wa kimataifa.

Kikosi hicho kinafaa kuingia baada ya hatamu ya ATMIS kuisha mwezi Disemba 2024.

Tayari wanajeshi chini ya kikosi hicho wameanza kuondoka.

Tume ya AU iliahidi katika mkutano huo wa Agosti 2024 kuendelea na mazungumzo ya kina na Umoja wa Mataifa, Muungano wa Ulaya na washirika wote ili kuhakikisha ufadhili wa kutosha, unaotabirika na endelevu na aina nyingine za usaidizi, kujaza mapengo ya kifedha, kwa AUSSOM.

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post