VIKOSI VYA ULINZI VYAPEWA ELIMU YA UCHAGUZI.MWANZA

 

Maafisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali 406 kutoka Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto, Uhamiaji, Mgambo na Polisi wasaidizi wamejengewa uwezo kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.


Elimu hiyo ya kusimamia uchaguzi imetolewa leo Jumamosi Agosti 24,2024, katika viwanja vya Mabatini jijini Mwanza na Mkuu wa  Mafunzo ya Polisi kutoka makao makuu ya Polisi Dodoma, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ally Lugendo alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. 


DCP Lugendo amesema elimu hiyo ni muhimu kwa watu wote hususan askari Polisi na vyombo vingine vya usalama ili kujijengea uwezo wa kuzielewa sheria za uchaguzi ambazo kwa mwaka huu zimefanyiwa maboresho ikiwemo Sheria namba moja ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka 2024.


Elimu hiyo imeambatana na matembezi ya hiari (route match) pamoja na mazoezi ya viungo yenye lengo la kuweka utimamu wa mwili na ushirikiano kwa askari wa vyombo hivyo vya usalama.


Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafungwa amesema mazoezi hayo ni yamuhimu sana kwani yanaimarisha afya na yanasaidia kupunguza msongo wa mawazo, hivyo ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wote walioshiriki na kuhamasisha kuendelea kujitokeza kwenye mazoezi hayo.



Mazoezi hayo yamefanyika ikiwa ni muendelezo wa mazoezi  ya pamoja yenye lengo la kujenga afya za askari na ushirikiano katika kubadilishana mawazo na uzoefu wa namna ya kukabiliana na matukio mbalimbali yanayoshughulikiwa na vyombo hivi vya ulinzi na usalama kutoka wizara ya mambo ya ndani ya nchi.



Na Pascal Kadushi
Post a Comment (0)
Previous Post Next Post