NI MUHIMU SANA KWA MWANANCHI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA.MRATIBU MATIA LEVI


 

Mratibu wa uchaguzi Mkoa wa Mwanza Matia Levi amefafanua kuhusu daftari la kudumu la mpiga kura ambapo amesema kuwa daftari hili ni daftari ambalo linakuwa na takwimu mbalimbali  za wapiga kura ikiwa ni pamoja na jina mahali na eneo ambalo mtu amejiandikishia .


Ameyasema hayo  kupitia kipindi cha mchakamchaka huku akisisitiza kuwa kuanzia tarehe 21 hadi 27 kutakuwa na uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura na baadaye kupatiwa vitambulisho kwa ajili ya uchaguzi mkuu hapo mwakani 2025


Aidha amehitimisha kwa kutoa mwongozo wa sifa za mtu ambae anapaswa kwenda kujiandikisha na daftari la kudumu la mpiga kura ambapo amesema umri ni kuanzia miaka 18 na kuendelea

Na Mary Makanza

Zaidi kumsikiliza tumekuwekea video hapa chini bofya kumskiliza



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post