SIMBA NA YANGA WATAINGIA NUSU FAINALI !

 


Hizi ndizo mechi za kibabe na Simba, Yanga wote wamesisitiza wako tayari kukiwasha Kwa Mkapa maarufu kama Lupaso. Mechi za kuonyesha ukubwa wa Simba na Yanga katika anga la kimataifa. Mechi za kuleta heshima Afrika.

Ndio, juzi jioni jijini Cairo, Misri ilifanyika droo ya mechi za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika na vigogo hivyo kupangwa na mabingwa wa Afrika.
Yanga imepangwa kukutana na mabingwa wa michuano mipya ya soka Afrika, African Football League (AFL), Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, ilihali watani wao wa jadi, Simba wakipewa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri.

Droo nyingine zilihusisha TP Mazembe ya DR Congo itakayokutana na Petro Atletico ya Angola wakati Esperance ya Tunisia itaumana na Asec Mimosas ya Ivory Coast.

Tangu kufanyika kwa droo hiyo, kumekuwa na mijadala na maoni tofauti kutoka kwa wadau wa klabu hizo mbili juu ya nafasi ya timu hizo kwenda nusu fainali.

Wapo wanaoamini Simba ina njia nyepesi kulingana na Yanga inayokutana na Mamelodi ambayo kwa misimu ya hivi karibuni imekuwa tishio zaidi katika soka la Afrika.

Hata hivyo, bado Simba na Yanga hazitakiwi kubweteka au kujikatia tamaa kutokana na kupangwa na vigogo hivyo vya soka la Afrika.
Soka ni mchezo wa maajabu na pia una matokeo ya kushangaza, ukibebwa zaidi na sayansi inayohusisha maandalizi mzuri, mbinu za kupambana ndani ya dakika 90 za kila pambano na bila ya kuisahau bahati. Ndio, bahati katika soka huzaa matokeo yasiyotarajiwa.
Pia soka la kisasa limeifuta ile dhana kwamba ni lazima timu wenyeji ipate matokeo mazuri nyumbani na kupoteza zile za ugenini na badala yake mambo yapo kinyume.
Maandalizi mazuri na mbinu bora zitazibeba timu bila kujali kama zinacheza ugenini au nyumbani, kitu ambacho Simba na Yanga lazima ziishi katika dhana hiyo ili kupenya mbele ya Mamelodi na Al Ahly na hapa chini Mwanaspoti linakuletea dondoo ambazo timu hizo zikiamua kukomaa nazo basi zina nafasi kubwa ya kuishangaza Afrika na kufuzu nusu fainali.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post