HASSAN MASALA AGEUKA MBOGO MBELE YA AFISA AFYA KUWAPORA MAMA NTILIE

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mwalimu Hassan Masala leo Tarehe 05.03.2024,Ameendelea na ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi katika wilaya yake yenye kata 19 Baada ya Kupita Kata ya Buswelu na Kiseke na Kusimama kwa Muda kufatia Msiba wa Taifa wa Rais wa Pili wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Hayati Ali Hassan Mwinyi aliyefariki tarehe 29.02.2024 Na Rais wa Awamu ya sita ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Samia suluhu Hassan Kutangaza Maombolezo ya siku Saba kwa Taifa.

Siku ya Jumanne ya tarehe 05 mach 2024 Ameendelea na ziara yake ya kusikiliza kero Katika Kata ya Kawekamo,Kubwa zaidi ni Afisa Afya wa kata ya Kawekamo Bwana Paul Nataniel  aliye changisha Shillingi 10,000 kwa wafanya Biashara wadogowadogo Maarufu kama Mama ntilie  na kuchukua pesa shillingi 100,000 na kukaa nazo ofisini kwake zaidi ya miezi miwili pasipo Kutolea Taarifa.





Tuhuma za kuchukua Pesa hizo kwa mama ntilie ziliibuliwa na mmoja ya wa wafanya biashara hao waliochukuliwa pesa zao Femia Bituro

Mama Ntilie-Femia Bituro

na Alipoulizwa Afisa huyo wa Afya na Mkuu huyo wa wilaya alisema anasubilia apate Namba ya Malipo (Control Number) ili hizo pesa aziweke kwenye Akaunt ya Serikali
Mkuu wa wilaya  Mwl Hassan Masala Akamtaka Afisa huyo wa Afya kwenda kuzichukua pesa hizo na majina ya watu wote waliochukuliwa pesa zao  kabla ya mkutano wake kumalizika
kwa lengo kuona namna gani Mama hao wanapewa pesa zao,Pamoja na hilo amewataka Viongozi wake wa juu kumchukulia Hatua za kinidhamu zaidi




AFISA AFYA WA KATA YA KAWEKAMO BW.PAUL NATANIEL AKIWAKILISHA PESA NA MAJINA YA MAMA NTILIE











Wakili Mariam Abubakar Msengi-Katibu tawala wa wilaya ya Ilemela
Akitolea Ufafanunzi wa kisheria baada ya mwananchi kutoa kero yake ya Ardhi.

Wakili Kibamba Kiamoni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela,Akitolea Ufafanunzi juu ya changamoto za barabara katika Manispaa ya ilemela ambazo mwarobaini wake wameupata,amesema siku za hivi karibuni wanategemea kupata mitambo yao ya ujenzi wa barabara. 



By Pascal Kadushi

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post